Alhamisi, 24 Oktoba 2013

Kujiunga

Unknown | 06:18 |

              Kujiunga

Beep Mara moja tu Kwenye no 0755 700 820 utapokea ujumbe wa maelekezo

Kuwaimarisha vijana kwenye Neno kwa njia mbalimbali za kuwafundisha, kufanya MAKONGAMANO Semina na mashindo yanayoweza kuibua vipawa na karama pamoja na maarifa Mungu Aliyoweka ndani yao, kutoa zawadi za pesa taslimu au vifaa ili kutia moyo vijana waamshe shauku  yao ya kusoma Neno na kulitafakari.
Kufikia nchi nzima ya Tanzania kupitia vijana waliookoka  ili  nao wawalete wengine kwa Yesu.
Kuanzisha mahubiri kwenye kila daladala/mabasi yote yanayofanya safari ndani ya nchi hii,kwa kuwa matatizo mengi yaliyomzunguka mwanadamu yanasababishwa na dhambi Rumi 2:9-11, hivyo kwa kutumia rasilimali watu  vijana wenye ufahamu mzuri hawa watakuwa waalimu, wainjilisti (wahubiri) wasimamizi wa miradi itakayo anzishwa ili kupiga vita Dhambi ufukara na Ujinga.

Kuhubiri Injili Kwa Njia ya Techkohama (ICT)
kuazisha tovuti na database kwa kila Kanisa na kumwaandaa kijana mmoja atakayeisimamia, na  kuingiza kumbukumbu pamoja na  kutoa ripoti wakati zinapohitaji. Mchungaji wa Kanisa la mahali pamoja ndiye atakayekuwa msimamizi mkuu kwa kuhakikisha kila kitu kipo sawa kabla ya kuwekwa hewani hasa data zote za website. Kuitumia website (Mtandao) kuwa chombo cha kupeleka Injili kwa kasi na kufikia vijana wa kizazi kipya cha dot com, Injili ni uweza wa Mungu hivyo unaweza kumfikia kila mtu na mahali popote na kwa wakati wowote, mimi na wewe tunawajibika kuipeleka Injili  kwa kila mtu, tunahitaji taaluma na Bwana kaiweka mikononi mwetu, tuitumie ili kutimiza malengo ya Mpango Mkakati wa Miaka Kumi Ya Mavuno Tanzania. Kutakuwa na website za aina mbili, (1.) Isiyo na gharama ila backup ya kila mwezi (2.) Yenye gharama kulingana na hitaji la Kanisa husika.

Huduma

Kwanza ningependa kusema kuwa hatuanzishi jambo jipya, bali ni kuboresha na kuongeza kasi kwenye huduma ya kuwafikia watu kwa Injili ya Yesu, kwa ubora, ubunifu na utaalamu wa hali ya juu.
kutembelea wagonjwa, wafungwa na wajane na Yatima. Kufikia mashule na vyuo kwa Injili ya Yesu na mengine mengi kwa kadri ya Neema ya Bwana, Huduma hii itafanya kwa kushirikiana na Kanisa la mahali kupitia idara ya vijana woca watakuwa wawezeshaji kuhakikisha lengo linatimia.
Uaminifu – kuifanya huduma hii kunahitaji uaminifu kwa Mungu na kwa wanadamu kwa kutumika bila kujali hali,mazingira wala muda, bali kujitoa kwa moyo na kwa nia iliyosafi, kitu ambacho kimekuwa mtihani mgumu kwa wengi.

Kutoa Ujunzi

Kufungua vyuo vya mafunzo ya ufundi kila jimbo, Section na Kwenye Kanisa la mahali kulingana na uhitaji wao, ili kutoa fursa kwa Vijana kujifunza na kukabiliana na soko la ajira duniani.
Maombi  saa:
6:00 hadi 7:00 mchana
9:00 hadi 10:00 jioni
12:00 hadi 1:00 usiku
9:00 hadi 11 alfajiri Kila siku
Mkesha saa 5:00 usiku hadi 9:00 Alfajiri kila ijumaa
Share this article

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Copyright © 2015 HEZRON MWANAFUNZI WA YESU • All Rights Reserved.
Blogger Templates Design by BTDesigner • Powered by Blogger