|
MWINJILISTI MWAKILIMA ATAHUBIRI |
Injili ya Yohana ina idadi kubwa tu ya ahadi za Yesu kuhusu
nafasi ya Roho Mtakatifu katika maisha ya waaminio. Hebu tusome baadhi
yake
.
Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi
hata milele. Ndiye Roho wa kweli, ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa
kuwa haumwoni wala haumtambui. Bali ninyi mnamtambua, maana anakaa
kwenu, naye atakuwa ndani yenu. - (Yohana 14:16, 17).
Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa
jina langu, atawafundisha yote na kuwakumbusha yote niliyowaambia
(Yohana 14:26).
Lakini mimi nawaambia iliyo kweli – yawafaa ninyi mimi niondoke. Kwa
maana, mimi nisipo-ondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu, bali mimi
nikienda zangu, nitampeleka kwenu. … Hata bado nikali ninayo mengi ya
kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili hivi sasa. Lakini yeye
atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote.
Kwa maana, hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia
atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake. Yeye atanitukuza
mimi, kwa kuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha habari.
Na yote
aliyo nayo Baba ni yangu, kwa hiyo nalisema ya kwamba atatwaa katika
yaliyo yangu na kuwapasheni habari (Yohana 16:7; 12 – 15)
read more...