Alhamisi, 31 Oktoba 2013

Unknown | 20:28 |

UKOMBOZI KILIMANJARO HAUKWEPEKI

Ni kama vile dozi ya injili imeshauriwa na Daktari Bingwa, maana baada ya uwanja wa mashujaa jijini Moshi mkoa wa Kilimanjaro kuhitimika kwa mkutano mkubwa wa kanisa la Utukufu wa Yesu, sasa viwanja hivyo vinapumua kwa siku chache tu kabla ya watumishi wengine kuendelea na ratiba ua injili.
Zamu hii wakati Ufufuo na Uzima wakiwa kwenye jengo ambalo watakuwa wakilitumia kama kanisa la mkoani humo, mtumishi wa Mungu kutoka Sweden, Mwinjilisti Johannes Amritzer atapiga kambi kwa takriban siku tano, kutakuwa na sherehe ya miujiza.


Pamoja na kuhubiri matendo makuu ya Mungu, waimbaji kadha wa kadha watakuwepo wakiwemo Anne Annie, Kilimanjaro Gospel Choir, na wengineo wengi. Kupanga kukosa ni sawa na kutoroka usipate uponyaji wako.

Share this article

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Copyright © 2015 HEZRON MWANAFUNZI WA YESU • All Rights Reserved.
Blogger Templates Design by BTDesigner • Powered by Blogger