Jumatano, 6 Novemba 2013

BWANA NDIE JIBU,MTATUAJI WA KILA AINA YA TATIZO. Sehemu ya 1

Unknown | 21:52 | Be the first to comment!


MTUMISHI WA BWANA KAKA HEZZO

read more...

Jumatatu, 4 Novemba 2013

MAISHA YA UKRISTO VITA SIO LELEMAMA,

Unknown | 22:32 | Be the first to comment!
Ni mimi ndugu yako Hezzo Daking  wa Maisha ya Ukristo Vita  sio   lelemama.Ni kufa  na  kupona.Tena  vita  vyetu sisi 


“si juu  ya  damu na  nyama bali  ni  juu  ya  falme  na  mamlaka  juu  ya  wakuu wa  giza  hili, juu  ya  majeshi  ya  pepo  wabaya  katika ulimwengu wa  roho “{Wafeso 6:12}.Vita  kali
Kuna  watu  wengi  wanaokata  shauri  kumpokea  YESU(wanaokoka).Kweli wanakuwa  wamepanga  hasa  kwenda  mbinguni.Wanaimba nyimbo  za  sifa zionyeshazo hamu  ya  kuwa YESU  arudi upesi.Huaanza kushuhudia kwa  nguvu zote,hata kwa  kufunga  na  kuomba na  machozi.Wanakuwa wameanza Vita wanakutana  na  vikwazo na  shida  njiani wanapigana  sana.Wengi wanashinda lakini wengine  wengi wanachoka  polepole  na  wanaachwa  na  wenzao  wanapobaki nyuma  peke,  yao adui anakuja  na  kuwazunguka  na  kuwateka  mateka

Pengine umekwisha waona  hawa  waliorudi nyuma  wakaanguka.Usidhani kuwa  mtu anayekata shaurikumwacha YESU huwa wanajishtukia wameanguka kushindwa huku ni  sawa na  usingizi.ukilala kitandani unakuwa ukiwaza mambo  mengi  au  unazungumza na mwenzako. 

La ajabu ni kwamba hujui unasinzia saa ngapi na  dakika ngapi na ukaacha kusikia hata  kama  utalala ukiangalia saa unayezungumza naye anakuja  kugundua kuwa anazungumza peke yake tu wewe unatambua kuwa ulikuwaumesinzia wakati unapoamka, 
ndivyo ilivyo kwa  maisha ya kiroho. Mtu hawezi  kujua lini hasa alipoanguka
Anakwenda  taratibu hatua  kwa  hatua akisogea  nyuma na baadaye anajikuta ameanguka amekwishatekwa na maadui

Maadui wetu wana  nguvu sana .Maadui hasa ni watatu

1. Adui wa kwanza ni  shetani:

ni kawaida watu wa MUNGU kusema shetani ameshindwa Haleluya’’.Ni kweli Lakini hakufa ili kwa vile ameshindwa na YESU amri jeshi mkuu amekimbia na kuzungukazunguka akikuta mtu amebaki  nyuma na amechoka basi anamteka tu Yeye shetani kama simba angurumaye huzungukazunguka akitafuta mtu ammeze -1 petro 5:8

Shetani siyo mvivu anashughulika  usiku na  mchana akiwatafuta watu wa MUNGU ili aende nao jehanamu Tusije tukasahau hili,
 Biblia anasema kwamba tukeshe {tukae macho } ili tumpinge atakapokuja kutushambulia.


Tuwe tumevaa silaha zote za MUNGU ili tupate kujikinga na kuzipinga hila zake {Wafeso 6:11}

2. Adui  wa pili ni mwili: 

Biblia inasema “mwili”, ina maana ya ule utu wa kale, ile hali ya dhambi tuliyonayo kwa asili.mwili hupambana na roho zetu Tena mwili huu {flesh} ni wa mauti.Paulo anaeleza vizuri jambo hili katika -Warumi 7:15-24

Upo uwezekano wa kuishi kufuatana na mapenzi ya mwili k.m kutamani kuona wivu kudanganya ili kukwepa hatari kutotii,n.k mwili upo karibu sana nasi tena ni sehemu yetu.Ni adui wa hatari sana tumchunge

3. Adui wa tatu ni ulimwengu

Ulimwengu  ni mambo yote yaliyo kinyume na MUNGU mambo ya dunia k.m miundo ya jamii,siasa,mazingira,watu n.k
Ulimwengu  una  dhiki BWANA hakutoa ahadi kwamba hatutapata dhiki -1thes.3:3,4 

Dhiki ni sehemu ya ukristo wetu Lakini ni vigumu kuvumilia dhiki kama njaa,uchi,ugongwa na uchungu wa kifo.Hata hivyo ugumu huu siyo  kisingizio cha kushindwa kwetu.

Ulimwengu hauna dhiki tu.Una raha pia.Raha nayo inaweza kabisa kutufanya tumwache BWANA kwa mfano Dema, ambaye Paulo alimwita mtendakazi pamoja nami alikaa  na  Paulo muda mrefu akihubiri .Lakini Paulo alipo fungwa gerezani tunashangaa tukiona anamwandikia mpendwa wake timotheo kwa masikitiko akisema 
“DEMA aliniacha ,akiupenda ulimwengu huu wa sasa -2timotheo 4:10
Alikwepa dhiki akakimbia raha wenzetu wengi wameangushwa na raha hizi kama mali,wapenzi, vyeo n.k wanasahau kabisa wito waliloitwa na BWANA
Hata hivyo maadui hawa wasitutishe.tunaye YESU,BWANA wa MAJESHI yule mwanamke aliyeitwa Hana, alishuhudia akisema 


“Wala hakuna mwamba kama MUNGU wetu “ {1samweli 2:22} 


Tunaweza  kujiunga naye tukiimba
Moyo wangu wamshangilia BWANA
Pembe  yangu imetukuka katika BWANA
Kinywa  changu kimepanuka juu  ya adui zangu
Kwa kuwa naufurahia wokovo wako {1samweli 2:1}
Tujue tuko. vitani vita vya kiroho, vya imani. tusiwe kama wajinga tukajisahau
Ndiyo maana Paulo ,akijaa ROHO MTAKATIFU anatwambia ,
"Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za MUNGU mpate kuweza kushindana siku ya uovu ,mkiisha kuyatimiza yote ,kusimama “{efeso 6:13}
Katika sehemu inayifuata, tujaribu kuona silaha hizi za MUNGU zitakazotuwezesha kumshinda  shetani, mwili na ulimwengu, na kukua kiroho.
MUNGU awabariki sana ndugu wote.


Ni mimi ndugu yako Hezzo Daking
read more...

MAITI NYINGINE YAFUFUKA HUKO GEITA....ALIJINYONGA KWA KAMBA MWAKA JANA ILA SASA APATIKANA AKIWA HAI.!!

Unknown | 03:33 | Be the first to comment!

HOFU imezidi kutanda kwa wakazi wa Mkoa wa Geita kufuatia matukio ya watu waliofariki dunia na kuzikwa miaka iliyopita kuibuka wakiwa hai, Uwazi lina mkasa mwingine mpya.
Mgonda Thomas (22), aliyefariki dunia kwa kujinyonga Mei 28, mwaka jana na kuzikwa siku iliyofuata, Ijumaa iliyopita aliibukia karibu na mlango wa nyumbani kwao akiwa hai.
Tukio hilo ambalo bado la moto, lilijiri katika Kijiji cha Rumasa, Kata ya Buseresere, wilayani  Chato mkoani Geita.
Kwa mujibu wa chanzo, majirani ndiyo waliomshuhudia Mgonda akitembea barabarani saa tisa alasiri hatua chache kutoka kwenye mlango wa nyumba hiyo huku nguo zake zikiwa zimechakaa.

Baba mzazi wa kijana huyo, mzee Thomas Msalaba (60) akizungumza na mwandishi wa habari hizi alisema majirani hao ndiyo waliomtaarifu kwamba mwanaye Mgonda alikuwa barabarani.
“Niliondoka kwenda kumshuhudia kama kweli ni mwanangu. Nilipofika, nilimchunguza kwa umakini sana na kubaini alikuwa yeye.

Alama kubwa iliyokuwa kwenye mwili wa mwanangu ni kovu kwenye mkono wake wa kushoto lililotokana na kuungua moto, pia sura yake ilifanana sana na mama yake,” alisema mzee huyo.
Naye mama mzazi wa Mgonda, Martha Kitobelo alimthibitishia paparazi wetu kuwa kijana huyo ni mwanaye kweli.
Familia hiyo ilisema Mgonda alifariki dunia kwa kujinyonga kwa kutumia kamba aliyoifunga juu ya mti wa mwembe hatua chache kutoka nyumbani kwao. Haikujulikana chanzo cha kujinyonga.

Mzee Msalaba alisema kuwa, baada ya Mgonda kufariki dunia alizikwa kwenye makaburi ya nyumbani kwao na siku ya tatu ndugu walianua matanga.
Kufuatia hali ya Mgonda kuwa ya mawengemawenge na kushindwa kuzungumza, wazazi wake walimchukua na kumpeleka kwa mganga wa kienyeji wa eneo hilo aitwaye Juma Tabiho.
Mganga huyo alisema kijana huyo hakufa bali alichukuliwa msukule na maiti waliyoizika ilikuwa kiini macho.
Hata hivyo, katika tukio hilo Jeshi la Polisi Wilaya ya Chato likiongozwa na Mrakibu wa Polisi Wilaya, OCD Leonard Nyaoga lililazimika kufanya kazi ya ziada kuwatuliza wananchi waliopandwa na hasira waliotaka kufukua kaburi ili kuona kilichokuwa ndani.

Afande Nyaoga aliwaambia wananchi hao kwamba kufanya hivyo ni kuvunja sheria za nchi na kuwaeleza kuwa chombo chenye uwezo wa kutoa kibali cha kufukua kaburi ni mahakama peke yake.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Pudensiana Protas alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema uchunguzi unaendelea ikiwa ni pamoja na kufanya utaratibu wa kumpima DNA kijana huyo ili kujiridhisha kama kweli ndiye Mgonda aliyefariki dunia mwaka jana.
Hili ni tukio la tatu kutokea mkoani Geita katika kipindi kisichozidi miaka mitano iliyopita.
Aprili 12, 2013 katika Kijiji cha Kasamwa wilayani Geita, Flora Onesmo (45) aliyefariki dunia Februari 28, 2008 aliibuka akiwa hai.

Septemba 28, mwaka huu aliyekuwa mwanafunzi wa darasa la tano katika Shule ya Msingi Mwatulole mjini Geita, Shaban Maulid (16) aliyefariki dunia  Januari 1, 2011 naye aliibukia Mtaa wa Mbugani jirani na nyumbani kwao, Kata ya 14, Kambarage mjini Geita.
Kufuatia matukio hayo yenye dalili za ushirikina, Askofu wa Kanisa la Zion Assemblies of God Geita, Edward Osako alisema katika maandiko hakuna binadamu aliyewahi kufa kisha akafufuka zaidi ya Lazaro aliyefufuliwa na Yesu akiwa kaburini.
Haya matukio ya watu kufa na kuonekana wakiwa hai baada ya miaka kadhaa ni nguvu za giza ambapo hata kwenye Biblia yameandikwa,” alisema Askofu Osako.

Read more: http://habarizabongo3.blogspot.com/2013/10/maiti-nyingine-yafufuka-huko.html#ixzz2jdl4JGAQ

read more...

Jumapili, 3 Novemba 2013

AAMUA KUJINYONGA KUKWEPA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE ,KISA HOFU YA KUFELI(,TUNAOMBA RADHI KWA PICHA HIZI)

Unknown | 23:26 | Be the first to comment!


 Mwanafunzi  aliyekuwa akisubiri kufanya  mtihani  wa kidato cha nne unaotaraji  kuanza kesho Bw Khamis Mkundo mkazi  wa Mwangata C katika Manispaa  ya Iringa  akiwa amejinyonga  usiku  huu kuhofu  mtihani  wa kidato cha nne

 Mwenyekiti  wa serikali ya mtaa wa Mwangata C Bw Sarehe Mgimwa akisoma ujumbe  ulioachwa na marehemu huyu
 Askari  kanzu  akikagua  mwili wa mwanafunzi  huyo  leo

 Wananchi  wa Mwangata  mjini Iringa  wakiwa nyumbani kwa marehemu  usiku  huu

 Mwili  wa kijana  huyo ukitolewa  tayari  kupelekwa  chumba  cha kuhifadhia maiti Hospital  ya  Rufaa ya mkoa  wa Iringa
Mwili  huo ukipakiwa katika gari  la  polisi
 

Mwanafunzi  wa  aliyekuwa akisoma  shule  ya  sekondari  Sabasaba  mjini  Iringa akijiandaa kurudia  kufanya  mtihani  wa  taifa  wa kidato  cha nne kupitia  kituo  cha Krelluu mjini  Iringa Khamis Mkundo  mkazi  wa Mwangata  C katika manispaa ya  Iringa amejiua kwa kujinyonga  kwa kamba kwa kile  alichodai  kuchoshwa na kufeli  mara kwa mara mtihani wa kidato cha nne.


Katika  barua  yake  ndewfu aliyoiandika  kijana  huyo amesema  kuwa amefanya  hivyo si kwa kujipendea  ila amechukizwa na hatua yake ya  kufeli mara kwa mara  hiyo  kuamua  kujiua ili  kuepuka na aibu katika mtihani ujao ambao anaamini angefeli.


Shemeji  wa  kijana  huyo Aden Tagalile ameueleza mtandao  huu  wa www.matukiodaima.com  kuwa  tukio  hilo limetokea mida ya  kati ya saa 12 na saa 1  usiku wa  leo baada ya kuwepo kwa mazungumzo ya muda  mrefu  kwa kijana  huyo kuonyesha kuchukia hatua yake ya kuendelea kuristi  mtihani  wa kidato cha nne  bila mafanikio.


Kwani  alisema hajapenda  kuona anaendelea  kufeli na kuwa  yupo tayari kwa lolote  kukwepa aibu ambayo ipo mbele  yake.


Hata  hivyo kufuatia mazungumzo hayo kijana huyo aliangana na ndugu zake akiwemo kaka  yake anayeishi nae kwa kila mmoja kuondoka nyumbani  hapo kabla  ya kijana  huyo kukutwa amejinyonga.


Mwenyekiti  wa serikali  ya mtaa huo Sarehe Mgimwa amethibitisha  kutokea kwa kifo  hicho na kuonyesha ujumbe ambao kijana  huyo ameuacha .


read more...

Jumamosi, 2 Novemba 2013

Unknown | 11:48 | Be the first to comment!

         

Wisdom for the Journey
Are You Hurting?
Discover a way to healing

"My Prayer for Today"
Lord, let me not underestimate myself. Whenever I am tempted to do so, may I remember that you have made me after your own image, whole and sacred, beautiful and with infinite potentials!
read more...

Ijumaa, 1 Novemba 2013

Unknown | 20:35 | Be the first to comment!

                    MAOMBI

Je una hitaji lolote ungependa kushirikisha watu/mtu kwa ajili ya kumuomba Mungu? yaweza liwe lako binafsi, nchi, watumishi wa Mungu na mengineyo. hezzodaking.blogsport.com Tuna Team ya Maombi ambapo tunaombea maombi haya. Pia Yeyote popote Ulipo unaweza kuguswa kumuombea mtu mahala hapa na akapokea Uponyaji kwa Jina la Yesu Kristo.

Ukipokea Uponyaji, Tutafurahi kupata ushuhuda wako. Karibuni

Kujiunga na Team ya maombi wasiliana nasi kwa

Email: hezzodaking6@gmail.com or call on +255767674089

read more...
Unknown | 07:01 | Be the first to comment!

CHUKUA TIME YAKO KUSOMA KILICHO ANDIKWA NA GAZETI LA JAMBO LEO KUHUSU TB JOSHUA.

 TB Joshua aliwahi kutabiri kifo cha Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe na kuibua mjadala mzito kwa nchi za Afrika na kifo cha Rais wa Nigeria, Umaru Yar’Adua na tukio la ugaidi nchini Marekani ambalo lilitokea mwaka 2001.
 ‘TB Joshua’, ametabiri kuwa, Rais mmoja wa nchi za Afrika Mashariki atatekwa na shambulizi la kigaidi kutokea katika nchi hizo.   Nchi za Afrika Mashariki kwa sasa zinaundwa na Uganda inayoongozwa na Rais Yoweri Museveni, Kenya inayoongozwa na Rais Uhuru Kenyatta, Rwanda na Rais Paul Kagame, Burundi ikiongozwa na Piere Nkurunzinza na Tanzania Rais Jakaya Kikwete. Utabiri huo umekuja siku chache baada ya TB Joshua kutabiri kifo cha Rais mmoja wa nchi za kusini mwa Afrika, ambapo haikuchukua muda kikatokea kifo cha Rais wa Malawi, Bingu wa Mutharika.
Pia, TB Joshua aliwahi kutabiri kifo cha Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe na kuibua mjadala mzito kwa nchi za Afrika na kifo cha Rais wa Nigeria, Umaru Yar’Adua na tukio la ugaidi nchini Marekani ambalo lilitokea mwaka 2001.
Mchungaji huyo wa Synagogue Church of All Nations (Scoan), alitoa utabiri wa rais mmoja wa Afrika Mashariki kutekwa mwezi uliopita mjini Nigeria, wakati akitoa mahubiri yake na kuacha taharuki kubwa kwa wananchi wa nchi hizo kuhusu ni rais gani atatekwa na shambulizi hilo litafanyika nchi ipi.
Akizungumza kwenye ibada hiyo kanisani kwake, Joshua alisema nchi ambayo ipo kwenye hatari ya kukutwa na tukio hilo ni ile iliyowahi kupatwa na matatizo wakati watu wake wakiwa wanakunywa na kucheza, huku akiongeza kwamba tukio hilo litatokea tena.
Ingawa hakutaka kutaja jina la kiongozi huyo wala nchi anayotokea, alisema ameambiwa na Mungu kwamba, endapo atamtaka kutaja jina la kiongozi na nchi atokayo, atafanya hivyo. Kutokana na hali hiyo, amewataka wananchi wa Afrika Mashariki kumuomba Mungu ili jambo hilo lisitokee.
Akitoa maoni kuhusu utabiri huo bila kutaja jina lake alisema: “imani ni hiyari. Yesu alituambia tutawajua kwa matunda yao, hivyo kama hufuatilii mahubiri ya TB Joshua na jinsi unabii wake unavyotimia, huwezi kuamini, lakini kama unafuatilia na bado huamini, basi muda wako kuamini haujatimia.
“Kama mnaamini unabii ulikuwepo, upo na utakuwepo hadi mwisho wa dunia, je, kwa nyie mnaobisha ni nabii gani mnayeamini ni mtumishi kweli wa Mungu?
“Manabii wapo na Mungu anaendelea kuleta miujiza kupitia wao ili tuamini kuwa,  yeye ndiye alfa na omega. Kama unasubiri nabii mpya azaliwe halafu wewe ndiyo useme huyu ndiyo nabii, basi subiri huo muujiza,” alisema.
TB Joshua ambaye ana wafuasi lukuki, aliwahi kutabiri kifo cha mfalme wa Pop duniani, Michael Jackson na kuangushwa kwa dikteta wa Ivory Coast, Laurent Gbagbo na kweli ikawa hivyo.
Alipoulizwa wakati mmoja ni kwa nini hupenda kutabiri mambo mabaya, alijitetea kwamba, anafanya hivyo ili kuwatahadharisha wanadamu kujiweka tayari kwa kufanya matendo mema.
TB Joshua aliwahi kutoa mchango wa sh.milioni 25 zikiwa ni rambirambi kwa watu wa Zanzibar waliopata ajali ya meli ya Spice Islander iliyotokea miaka michache iliyopita katika bahari ya Hindi na kupoteza maisha ya zaidi ya watu 240.   Nabii Joshua  amekuwa na msaada mkubwa Nigeria, kwa watu wa mataifa mbalimbali kiroho na kimwili, ikiwa ni pamoja kutoa misaada kwa jamii. Husaidia wajane, yatima, walemavu na maskini na humrudishia Mungu utukufu kwa kila jambo linalotokea kanisani kwake.
Katika kanisa lake watu wanaokwenda kupata ibada, hupata maji ya upako ambayo watu huyachukua na kuyatumia katika maombezi yao na wengi wameshuhudia kufunguliwa katika matatizo yao.   Muft Simba
Wakati huo huo, Magendela Hamisi anaripoti kuwa, Muft wa Tanzania, Sheikh Issa Shaban bin Simba ameishauri Serikali kuwalinda wananchi wake sanjari na viongozi mbalimbali wakiwemo wa dini kujilinda na changamoto hiyo.
Alitoa kauli hiyo Dar es Salaam jana baada ya kujibu swali lililomtaka kuweka wazi namna Waislamu wakatakavyoweza kujilinda katika mikusanyiko yao katika shughuli za ibada na nyinginezo kutokana na tishio la kigaidi lililopo katika nchi za Afrika Mashariki.
“Katika suala la kujilinda kutokana na tishio la kigaidi tunaichia Serikali, nikiamini kuwa ina wajibu mkubwa wa kufanya hivyo, lakini pia tunahitaji kuisaidia kwa kutoa taarifa zinazoashiria hayo.
“Hatujilindi kwa vita wala kujibu kutokana na matukio ya kigaidi na hatutaacha kufanya ibada kutokana na kuwepo kwa hali hiyo, tunaomba Serikali ijitahidi kuweka ulinzi kwa kuwalinda watu wake, nasi tunahitaji kuisaidia ili kulinda amani ya nchi yetu,” alisema.
Mufti Simba aliweka wazi kuwa katika shughuli hiyo ya kutimiza ibada ya Hijja, Mtanzania mmoja kutoka Mkoa wa Singida alipata matatizo ya afya baada ya kupata tatizo la ubongo lakini alihudumiwa vema na madaktari.   Alifafanua kuwa afya ya muumini huyo inaendelea vema na tayari amerejeshwa nchini kuendelea na matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) hadi hali yake itakapotengemaa.
Simba aliongeza kuwa licha ya dosari hiyo kujitokeza Hijja ya mwaka huu imefanikiwa kwa kiasi kikubwa na kuwa sehemu ya kujivunia na kuishukuru Serikali ya Tanzania kwa kufanikisha safari hiyo muhimu.   Pia Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum alisema ni vizuri Waislamu wote nchini wakaendelea kudumisha amani na utulivu na kuishi kwa upendo na jamii mbalimbali bila kujali tofauti za dini.
“Waislamu wote waliokuwepo Makkah waliishi kwa upendo na watu wa mataifa mbalimbali duniani hali ambayo inapaswa kuendelezwa nchini ili kudumisha amani na utulivu uliopo kwa maslahi ya taifa,” alisema.
Source: Jambo leo
read more...
 
Copyright © 2015 HEZRON MWANAFUNZI WA YESU • All Rights Reserved.
Blogger Templates Design by BTDesigner • Powered by Blogger