Jumatano, 6 Novemba 2013
Jumatatu, 4 Novemba 2013
MAISHA YA UKRISTO VITA SIO LELEMAMA,
Unknown | 22:32 |
HEZZO DAKING
Be the first to comment!
Ni mimi ndugu yako Hezzo Daking wa Maisha ya Ukristo Vita sio
lelemama.Ni kufa na kupona.Tena
vita vyetu sisi
Kuna watu
wengi wanaokata shauri
kumpokea YESU(wanaokoka).Kweli
wanakuwa wamepanga hasa
kwenda mbinguni.Wanaimba
nyimbo za sifa zionyeshazo hamu ya
kuwa YESU arudi upesi.Huaanza kushuhudia
kwa nguvu zote,hata kwa kufunga
na kuomba na machozi.Wanakuwa wameanza Vita
wanakutana na vikwazo na
shida njiani wanapigana sana.Wengi wanashinda lakini wengine wengi wanachoka polepole
na wanaachwa na
wenzao wanapobaki nyuma peke,
yao adui anakuja na kuwazunguka
na kuwateka mateka
read more...
“si juu ya damu na nyama bali ni juu ya falme na mamlaka juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho “{Wafeso 6:12}.Vita kali
Kuna watu
wengi wanaokata shauri
kumpokea YESU(wanaokoka).Kweli
wanakuwa wamepanga hasa
kwenda mbinguni.Wanaimba
nyimbo za sifa zionyeshazo hamu ya
kuwa YESU arudi upesi.Huaanza kushuhudia
kwa nguvu zote,hata kwa kufunga
na kuomba na machozi.Wanakuwa wameanza Vita
wanakutana na vikwazo na
shida njiani wanapigana sana.Wengi wanashinda lakini wengine wengi wanachoka polepole
na wanaachwa na
wenzao wanapobaki nyuma peke,
yao adui anakuja na kuwazunguka
na kuwateka mateka
Pengine
umekwisha waona hawa waliorudi nyuma wakaanguka.Usidhani kuwa mtu anayekata shaurikumwacha YESU huwa
wanajishtukia wameanguka kushindwa huku ni
sawa na usingizi.ukilala
kitandani unakuwa ukiwaza mambo
mengi au unazungumza na mwenzako.
La ajabu ni kwamba hujui unasinzia saa ngapi na dakika ngapi na ukaacha kusikia hata kama utalala ukiangalia saa unayezungumza naye anakuja kugundua kuwa anazungumza peke yake tu wewe unatambua kuwa ulikuwaumesinzia wakati unapoamka,
La ajabu ni kwamba hujui unasinzia saa ngapi na dakika ngapi na ukaacha kusikia hata kama utalala ukiangalia saa unayezungumza naye anakuja kugundua kuwa anazungumza peke yake tu wewe unatambua kuwa ulikuwaumesinzia wakati unapoamka,
ndivyo
ilivyo kwa maisha ya kiroho. Mtu
hawezi kujua lini hasa alipoanguka
Anakwenda taratibu hatua kwa
hatua akisogea nyuma na baadaye
anajikuta ameanguka amekwishatekwa na maadui
Maadui wetu
wana nguvu sana .Maadui hasa ni watatu
1. Adui wa kwanza ni shetani:
ni kawaida watu wa MUNGU kusema shetani ameshindwa Haleluya’’.Ni kweli Lakini hakufa ili kwa vile ameshindwa na YESU amri jeshi mkuu amekimbia na kuzungukazunguka akikuta mtu amebaki nyuma na amechoka basi anamteka tu Yeye shetani kama simba angurumaye huzungukazunguka akitafuta mtu ammeze -1 petro 5:8
Shetani siyo
mvivu anashughulika usiku na mchana akiwatafuta watu wa MUNGU ili aende
nao jehanamu Tusije tukasahau hili,
Biblia anasema kwamba tukeshe {tukae macho }
ili tumpinge atakapokuja kutushambulia.
Tuwe tumevaa silaha zote za MUNGU ili tupate kujikinga na kuzipinga hila zake {Wafeso 6:11}
2. Adui wa pili ni mwili:
Biblia inasema “mwili”, ina maana ya ule utu wa kale, ile hali ya dhambi tuliyonayo kwa asili.mwili hupambana na roho zetu Tena mwili huu {flesh} ni wa mauti.Paulo anaeleza vizuri jambo hili katika -Warumi 7:15-24
Upo
uwezekano wa kuishi kufuatana na mapenzi ya mwili k.m kutamani kuona wivu
kudanganya ili kukwepa hatari kutotii,n.k mwili upo karibu sana nasi tena ni
sehemu yetu.Ni adui wa hatari sana tumchunge
3. Adui wa tatu ni ulimwengu
Ulimwengu ni mambo yote yaliyo kinyume na MUNGU mambo
ya dunia k.m miundo ya jamii,siasa,mazingira,watu n.k
Ulimwengu una
dhiki BWANA hakutoa ahadi kwamba hatutapata dhiki -1thes.3:3,4
Dhiki ni sehemu ya ukristo wetu Lakini ni vigumu kuvumilia dhiki kama njaa,uchi,ugongwa na uchungu wa kifo.Hata hivyo ugumu huu siyo kisingizio cha kushindwa kwetu.
Dhiki ni sehemu ya ukristo wetu Lakini ni vigumu kuvumilia dhiki kama njaa,uchi,ugongwa na uchungu wa kifo.Hata hivyo ugumu huu siyo kisingizio cha kushindwa kwetu.
Ulimwengu
hauna dhiki tu.Una raha pia.Raha nayo inaweza kabisa kutufanya tumwache BWANA
kwa mfano Dema, ambaye Paulo alimwita mtendakazi pamoja nami alikaa na
Paulo muda mrefu akihubiri .Lakini Paulo alipo fungwa gerezani
tunashangaa tukiona anamwandikia mpendwa wake timotheo kwa masikitiko akisema
“DEMA aliniacha ,akiupenda ulimwengu huu wa sasa -2timotheo 4:10
Alikwepa
dhiki akakimbia raha wenzetu wengi wameangushwa na raha hizi kama mali,wapenzi,
vyeo n.k wanasahau kabisa wito waliloitwa na BWANA
Hata hivyo
maadui hawa wasitutishe.tunaye YESU,BWANA wa MAJESHI yule mwanamke aliyeitwa Hana,
alishuhudia akisema
Tunaweza kujiunga naye tukiimba
“Wala hakuna mwamba kama MUNGU wetu “ {1samweli 2:22}
Tunaweza kujiunga naye tukiimba
Moyo wangu
wamshangilia BWANA
Pembe yangu imetukuka katika BWANA
Kinywa changu kimepanuka juu ya adui zangu
Kwa kuwa
naufurahia wokovo wako {1samweli 2:1}
Tujue tuko.
vitani vita vya kiroho, vya imani. tusiwe kama wajinga tukajisahau
Ndiyo maana
Paulo ,akijaa ROHO MTAKATIFU anatwambia ,
"Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za MUNGU mpate kuweza kushindana siku ya uovu ,mkiisha kuyatimiza yote ,kusimama “{efeso 6:13}
Katika
sehemu inayifuata, tujaribu kuona silaha hizi za MUNGU zitakazotuwezesha
kumshinda shetani, mwili na ulimwengu,
na kukua kiroho.
MUNGU awabariki sana ndugu wote.
Ni mimi ndugu yako Hezzo Daking
MUNGU awabariki sana ndugu wote.
Ni mimi ndugu yako Hezzo Daking
MAITI NYINGINE YAFUFUKA HUKO GEITA....ALIJINYONGA KWA KAMBA MWAKA JANA ILA SASA APATIKANA AKIWA HAI.!!
Unknown | 03:33 |
HABARI
Be the first to comment!

HOFU imezidi kutanda kwa wakazi wa Mkoa wa Geita kufuatia matukio ya watu waliofariki dunia na kuzikwa miaka iliyopita kuibuka wakiwa hai, Uwazi lina mkasa mwingine mpya.
Mgonda Thomas (22), aliyefariki dunia kwa kujinyonga Mei 28, mwaka jana na kuzikwa siku iliyofuata, Ijumaa iliyopita aliibukia karibu na mlango wa nyumbani kwao akiwa hai.
Tukio hilo ambalo bado la moto, lilijiri katika Kijiji cha Rumasa, Kata ya Buseresere, wilayani Chato mkoani Geita.
Kwa mujibu wa chanzo, majirani ndiyo waliomshuhudia Mgonda akitembea barabarani saa tisa alasiri hatua chache kutoka kwenye mlango wa nyumba hiyo huku nguo zake zikiwa zimechakaa.
Baba mzazi wa kijana huyo, mzee Thomas Msalaba (60) akizungumza na mwandishi wa habari hizi alisema majirani hao ndiyo waliomtaarifu kwamba mwanaye Mgonda alikuwa barabarani.
“Niliondoka kwenda kumshuhudia kama kweli ni mwanangu. Nilipofika, nilimchunguza kwa umakini sana na kubaini alikuwa yeye.
“Alama kubwa iliyokuwa kwenye mwili wa mwanangu ni kovu kwenye mkono wake wa kushoto lililotokana na kuungua moto, pia sura yake ilifanana sana na mama yake,” alisema mzee huyo.
Naye mama mzazi wa Mgonda, Martha Kitobelo alimthibitishia paparazi wetu kuwa kijana huyo ni mwanaye kweli.
Familia hiyo ilisema Mgonda alifariki dunia kwa kujinyonga kwa kutumia kamba aliyoifunga juu ya mti wa mwembe hatua chache kutoka nyumbani kwao. Haikujulikana chanzo cha kujinyonga.
Mzee Msalaba alisema kuwa, baada ya Mgonda kufariki dunia alizikwa kwenye makaburi ya nyumbani kwao na siku ya tatu ndugu walianua matanga.
Kufuatia hali ya Mgonda kuwa ya mawengemawenge na kushindwa kuzungumza, wazazi wake walimchukua na kumpeleka kwa mganga wa kienyeji wa eneo hilo aitwaye Juma Tabiho.
Mganga huyo alisema kijana huyo hakufa bali alichukuliwa msukule na maiti waliyoizika ilikuwa kiini macho.
Hata hivyo, katika tukio hilo Jeshi la Polisi Wilaya ya Chato likiongozwa na Mrakibu wa Polisi Wilaya, OCD Leonard Nyaoga lililazimika kufanya kazi ya ziada kuwatuliza wananchi waliopandwa na hasira waliotaka kufukua kaburi ili kuona kilichokuwa ndani.
Afande Nyaoga aliwaambia wananchi hao kwamba kufanya hivyo ni kuvunja sheria za nchi na kuwaeleza kuwa chombo chenye uwezo wa kutoa kibali cha kufukua kaburi ni mahakama peke yake.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Pudensiana Protas alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema uchunguzi unaendelea ikiwa ni pamoja na kufanya utaratibu wa kumpima DNA kijana huyo ili kujiridhisha kama kweli ndiye Mgonda aliyefariki dunia mwaka jana.
Hili ni tukio la tatu kutokea mkoani Geita katika kipindi kisichozidi miaka mitano iliyopita.
Aprili 12, 2013 katika Kijiji cha Kasamwa wilayani Geita, Flora Onesmo (45) aliyefariki dunia Februari 28, 2008 aliibuka akiwa hai.
Septemba 28, mwaka huu aliyekuwa mwanafunzi wa darasa la tano katika Shule ya Msingi Mwatulole mjini Geita, Shaban Maulid (16) aliyefariki dunia Januari 1, 2011 naye aliibukia Mtaa wa Mbugani jirani na nyumbani kwao, Kata ya 14, Kambarage mjini Geita.
Kufuatia matukio hayo yenye dalili za ushirikina, Askofu wa Kanisa la Zion Assemblies of God Geita, Edward Osako alisema katika maandiko hakuna binadamu aliyewahi kufa kisha akafufuka zaidi ya Lazaro aliyefufuliwa na Yesu akiwa kaburini.
“Haya matukio ya watu kufa na kuonekana wakiwa hai baada ya miaka kadhaa ni nguvu za giza ambapo hata kwenye Biblia yameandikwa,” alisema Askofu Osako.
Read more: http://habarizabongo3.blogspot.com/2013/10/maiti-nyingine-yafufuka-huko.html#ixzz2jdl4JGAQ
Jumapili, 3 Novemba 2013
AAMUA KUJINYONGA KUKWEPA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE ,KISA HOFU YA KUFELI(,TUNAOMBA RADHI KWA PICHA HIZI)
Unknown | 23:26 |
HEZZO DAKING
Be the first to comment!
Mwanafunzi aliyekuwa akisubiri kufanya mtihani wa kidato cha nne unaotaraji kuanza kesho Bw Khamis Mkundo mkazi wa Mwangata C katika Manispaa ya Iringa akiwa amejinyonga usiku huu kuhofu mtihani wa kidato cha nne
Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Mwangata C Bw Sarehe Mgimwa akisoma ujumbe ulioachwa na marehemu huyu
Askari kanzu akikagua mwili wa mwanafunzi huyo leo
Wananchi wa Mwangata mjini Iringa wakiwa nyumbani kwa marehemu usiku huu
Mwili wa kijana huyo ukitolewa tayari kupelekwa chumba cha kuhifadhia maiti Hospital ya Rufaa ya mkoa wa Iringa
| Mwili huo ukipakiwa katika gari la polisi |
Mwanafunzi wa aliyekuwa akisoma shule ya sekondari Sabasaba mjini Iringa akijiandaa kurudia kufanya mtihani wa taifa wa kidato cha nne kupitia kituo cha Krelluu mjini Iringa Khamis Mkundo mkazi wa Mwangata C katika manispaa ya Iringa amejiua kwa kujinyonga kwa kamba kwa kile alichodai kuchoshwa na kufeli mara kwa mara mtihani wa kidato cha nne.
Katika barua yake ndewfu aliyoiandika kijana huyo amesema kuwa amefanya hivyo si kwa kujipendea ila amechukizwa na hatua yake ya kufeli mara kwa mara hiyo kuamua kujiua ili kuepuka na aibu katika mtihani ujao ambao anaamini angefeli.
Shemeji wa kijana huyo Aden Tagalile ameueleza mtandao huu wa www.matukiodaima.com kuwa tukio hilo limetokea mida ya kati ya saa 12 na saa 1 usiku wa leo baada ya kuwepo kwa mazungumzo ya muda mrefu kwa kijana huyo kuonyesha kuchukia hatua yake ya kuendelea kuristi mtihani wa kidato cha nne bila mafanikio.
Kwani alisema hajapenda kuona anaendelea kufeli na kuwa yupo tayari kwa lolote kukwepa aibu ambayo ipo mbele yake.
Hata hivyo kufuatia mazungumzo hayo kijana huyo aliangana na ndugu zake akiwemo kaka yake anayeishi nae kwa kila mmoja kuondoka nyumbani hapo kabla ya kijana huyo kukutwa amejinyonga.
Mwenyekiti wa serikali ya mtaa huo Sarehe Mgimwa amethibitisha kutokea kwa kifo hicho na kuonyesha ujumbe ambao kijana huyo ameuacha .
Jumamosi, 2 Novemba 2013
Unknown | 11:48 |
HEZZO DAKING
Be the first to comment!
"My Prayer for Today"
Ijumaa, 1 Novemba 2013
Unknown | 20:35 |
HEZZO DAKING
Be the first to comment!
MAOMBI
Je una hitaji lolote ungependa kushirikisha watu/mtu kwa ajili ya kumuomba Mungu? yaweza liwe lako binafsi, nchi, watumishi wa Mungu na mengineyo. hezzodaking.blogsport.com Tuna Team ya Maombi ambapo tunaombea maombi haya. Pia Yeyote popote Ulipo unaweza kuguswa kumuombea mtu mahala hapa na akapokea Uponyaji kwa Jina la Yesu Kristo.
Ukipokea Uponyaji, Tutafurahi kupata ushuhuda wako. Karibuni
Kujiunga na Team ya maombi wasiliana nasi kwa
Email: hezzodaking6@gmail.com or call on
Unknown | 07:01 |
HEZZO DAKING
Be the first to comment!
CHUKUA TIME YAKO KUSOMA KILICHO ANDIKWA NA GAZETI LA JAMBO LEO KUHUSU TB JOSHUA.
TB Joshua aliwahi kutabiri kifo cha Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe na
kuibua mjadala mzito kwa nchi za Afrika na kifo cha Rais wa Nigeria,
Umaru Yar’Adua na tukio la ugaidi nchini Marekani ambalo lilitokea mwaka
2001.
‘TB Joshua’, ametabiri kuwa, Rais mmoja wa nchi za Afrika Mashariki
atatekwa na shambulizi la kigaidi kutokea katika nchi hizo. Nchi za
Afrika Mashariki kwa sasa zinaundwa na Uganda inayoongozwa na Rais
Yoweri Museveni, Kenya inayoongozwa na Rais Uhuru Kenyatta, Rwanda na
Rais Paul Kagame, Burundi ikiongozwa na Piere Nkurunzinza na Tanzania
Rais Jakaya Kikwete.
Utabiri huo umekuja siku chache baada ya TB Joshua kutabiri kifo cha
Rais mmoja wa nchi za kusini mwa Afrika, ambapo haikuchukua muda
kikatokea kifo cha Rais wa Malawi, Bingu wa Mutharika.
Pia, TB Joshua aliwahi kutabiri kifo cha Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe na kuibua mjadala mzito kwa nchi za Afrika na kifo cha Rais wa Nigeria, Umaru Yar’Adua na tukio la ugaidi nchini Marekani ambalo lilitokea mwaka 2001.
Mchungaji huyo wa Synagogue Church of All Nations (Scoan), alitoa utabiri wa rais mmoja wa Afrika Mashariki kutekwa mwezi uliopita mjini Nigeria, wakati akitoa mahubiri yake na kuacha taharuki kubwa kwa wananchi wa nchi hizo kuhusu ni rais gani atatekwa na shambulizi hilo litafanyika nchi ipi.
Akizungumza kwenye ibada hiyo kanisani kwake, Joshua alisema nchi ambayo ipo kwenye hatari ya kukutwa na tukio hilo ni ile iliyowahi kupatwa na matatizo wakati watu wake wakiwa wanakunywa na kucheza, huku akiongeza kwamba tukio hilo litatokea tena.
Ingawa hakutaka kutaja jina la kiongozi huyo wala nchi anayotokea, alisema ameambiwa na Mungu kwamba, endapo atamtaka kutaja jina la kiongozi na nchi atokayo, atafanya hivyo. Kutokana na hali hiyo, amewataka wananchi wa Afrika Mashariki kumuomba Mungu ili jambo hilo lisitokee.
Akitoa maoni kuhusu utabiri huo bila kutaja jina lake alisema: “imani ni hiyari. Yesu alituambia tutawajua kwa matunda yao, hivyo kama hufuatilii mahubiri ya TB Joshua na jinsi unabii wake unavyotimia, huwezi kuamini, lakini kama unafuatilia na bado huamini, basi muda wako kuamini haujatimia.
“Kama mnaamini unabii ulikuwepo, upo na utakuwepo hadi mwisho wa dunia, je, kwa nyie mnaobisha ni nabii gani mnayeamini ni mtumishi kweli wa Mungu?
“Manabii wapo na Mungu anaendelea kuleta miujiza kupitia wao ili tuamini kuwa, yeye ndiye alfa na omega. Kama unasubiri nabii mpya azaliwe halafu wewe ndiyo useme huyu ndiyo nabii, basi subiri huo muujiza,” alisema.
TB Joshua ambaye ana wafuasi lukuki, aliwahi kutabiri kifo cha mfalme wa Pop duniani, Michael Jackson na kuangushwa kwa dikteta wa Ivory Coast, Laurent Gbagbo na kweli ikawa hivyo.
Alipoulizwa wakati mmoja ni kwa nini hupenda kutabiri mambo mabaya, alijitetea kwamba, anafanya hivyo ili kuwatahadharisha wanadamu kujiweka tayari kwa kufanya matendo mema.
TB Joshua aliwahi kutoa mchango wa sh.milioni 25 zikiwa ni rambirambi kwa watu wa Zanzibar waliopata ajali ya meli ya Spice Islander iliyotokea miaka michache iliyopita katika bahari ya Hindi na kupoteza maisha ya zaidi ya watu 240. Nabii Joshua amekuwa na msaada mkubwa Nigeria, kwa watu wa mataifa mbalimbali kiroho na kimwili, ikiwa ni pamoja kutoa misaada kwa jamii. Husaidia wajane, yatima, walemavu na maskini na humrudishia Mungu utukufu kwa kila jambo linalotokea kanisani kwake.
Katika kanisa lake watu wanaokwenda kupata ibada, hupata maji ya upako ambayo watu huyachukua na kuyatumia katika maombezi yao na wengi wameshuhudia kufunguliwa katika matatizo yao. Muft Simba
Wakati huo huo, Magendela Hamisi anaripoti kuwa, Muft wa Tanzania, Sheikh Issa Shaban bin Simba ameishauri Serikali kuwalinda wananchi wake sanjari na viongozi mbalimbali wakiwemo wa dini kujilinda na changamoto hiyo.
Alitoa kauli hiyo Dar es Salaam jana baada ya kujibu swali lililomtaka kuweka wazi namna Waislamu wakatakavyoweza kujilinda katika mikusanyiko yao katika shughuli za ibada na nyinginezo kutokana na tishio la kigaidi lililopo katika nchi za Afrika Mashariki.
“Katika suala la kujilinda kutokana na tishio la kigaidi tunaichia Serikali, nikiamini kuwa ina wajibu mkubwa wa kufanya hivyo, lakini pia tunahitaji kuisaidia kwa kutoa taarifa zinazoashiria hayo.
“Hatujilindi kwa vita wala kujibu kutokana na matukio ya kigaidi na hatutaacha kufanya ibada kutokana na kuwepo kwa hali hiyo, tunaomba Serikali ijitahidi kuweka ulinzi kwa kuwalinda watu wake, nasi tunahitaji kuisaidia ili kulinda amani ya nchi yetu,” alisema.
Mufti Simba aliweka wazi kuwa katika shughuli hiyo ya kutimiza ibada ya Hijja, Mtanzania mmoja kutoka Mkoa wa Singida alipata matatizo ya afya baada ya kupata tatizo la ubongo lakini alihudumiwa vema na madaktari. Alifafanua kuwa afya ya muumini huyo inaendelea vema na tayari amerejeshwa nchini kuendelea na matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) hadi hali yake itakapotengemaa.
Simba aliongeza kuwa licha ya dosari hiyo kujitokeza Hijja ya mwaka huu imefanikiwa kwa kiasi kikubwa na kuwa sehemu ya kujivunia na kuishukuru Serikali ya Tanzania kwa kufanikisha safari hiyo muhimu. Pia Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum alisema ni vizuri Waislamu wote nchini wakaendelea kudumisha amani na utulivu na kuishi kwa upendo na jamii mbalimbali bila kujali tofauti za dini.
“Waislamu wote waliokuwepo Makkah waliishi kwa upendo na watu wa mataifa mbalimbali duniani hali ambayo inapaswa kuendelezwa nchini ili kudumisha amani na utulivu uliopo kwa maslahi ya taifa,” alisema.
Pia, TB Joshua aliwahi kutabiri kifo cha Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe na kuibua mjadala mzito kwa nchi za Afrika na kifo cha Rais wa Nigeria, Umaru Yar’Adua na tukio la ugaidi nchini Marekani ambalo lilitokea mwaka 2001.
Mchungaji huyo wa Synagogue Church of All Nations (Scoan), alitoa utabiri wa rais mmoja wa Afrika Mashariki kutekwa mwezi uliopita mjini Nigeria, wakati akitoa mahubiri yake na kuacha taharuki kubwa kwa wananchi wa nchi hizo kuhusu ni rais gani atatekwa na shambulizi hilo litafanyika nchi ipi.
Akizungumza kwenye ibada hiyo kanisani kwake, Joshua alisema nchi ambayo ipo kwenye hatari ya kukutwa na tukio hilo ni ile iliyowahi kupatwa na matatizo wakati watu wake wakiwa wanakunywa na kucheza, huku akiongeza kwamba tukio hilo litatokea tena.
Ingawa hakutaka kutaja jina la kiongozi huyo wala nchi anayotokea, alisema ameambiwa na Mungu kwamba, endapo atamtaka kutaja jina la kiongozi na nchi atokayo, atafanya hivyo. Kutokana na hali hiyo, amewataka wananchi wa Afrika Mashariki kumuomba Mungu ili jambo hilo lisitokee.
Akitoa maoni kuhusu utabiri huo bila kutaja jina lake alisema: “imani ni hiyari. Yesu alituambia tutawajua kwa matunda yao, hivyo kama hufuatilii mahubiri ya TB Joshua na jinsi unabii wake unavyotimia, huwezi kuamini, lakini kama unafuatilia na bado huamini, basi muda wako kuamini haujatimia.
“Kama mnaamini unabii ulikuwepo, upo na utakuwepo hadi mwisho wa dunia, je, kwa nyie mnaobisha ni nabii gani mnayeamini ni mtumishi kweli wa Mungu?
“Manabii wapo na Mungu anaendelea kuleta miujiza kupitia wao ili tuamini kuwa, yeye ndiye alfa na omega. Kama unasubiri nabii mpya azaliwe halafu wewe ndiyo useme huyu ndiyo nabii, basi subiri huo muujiza,” alisema.
TB Joshua ambaye ana wafuasi lukuki, aliwahi kutabiri kifo cha mfalme wa Pop duniani, Michael Jackson na kuangushwa kwa dikteta wa Ivory Coast, Laurent Gbagbo na kweli ikawa hivyo.
Alipoulizwa wakati mmoja ni kwa nini hupenda kutabiri mambo mabaya, alijitetea kwamba, anafanya hivyo ili kuwatahadharisha wanadamu kujiweka tayari kwa kufanya matendo mema.
TB Joshua aliwahi kutoa mchango wa sh.milioni 25 zikiwa ni rambirambi kwa watu wa Zanzibar waliopata ajali ya meli ya Spice Islander iliyotokea miaka michache iliyopita katika bahari ya Hindi na kupoteza maisha ya zaidi ya watu 240. Nabii Joshua amekuwa na msaada mkubwa Nigeria, kwa watu wa mataifa mbalimbali kiroho na kimwili, ikiwa ni pamoja kutoa misaada kwa jamii. Husaidia wajane, yatima, walemavu na maskini na humrudishia Mungu utukufu kwa kila jambo linalotokea kanisani kwake.
Katika kanisa lake watu wanaokwenda kupata ibada, hupata maji ya upako ambayo watu huyachukua na kuyatumia katika maombezi yao na wengi wameshuhudia kufunguliwa katika matatizo yao. Muft Simba
Wakati huo huo, Magendela Hamisi anaripoti kuwa, Muft wa Tanzania, Sheikh Issa Shaban bin Simba ameishauri Serikali kuwalinda wananchi wake sanjari na viongozi mbalimbali wakiwemo wa dini kujilinda na changamoto hiyo.
Alitoa kauli hiyo Dar es Salaam jana baada ya kujibu swali lililomtaka kuweka wazi namna Waislamu wakatakavyoweza kujilinda katika mikusanyiko yao katika shughuli za ibada na nyinginezo kutokana na tishio la kigaidi lililopo katika nchi za Afrika Mashariki.
“Katika suala la kujilinda kutokana na tishio la kigaidi tunaichia Serikali, nikiamini kuwa ina wajibu mkubwa wa kufanya hivyo, lakini pia tunahitaji kuisaidia kwa kutoa taarifa zinazoashiria hayo.
“Hatujilindi kwa vita wala kujibu kutokana na matukio ya kigaidi na hatutaacha kufanya ibada kutokana na kuwepo kwa hali hiyo, tunaomba Serikali ijitahidi kuweka ulinzi kwa kuwalinda watu wake, nasi tunahitaji kuisaidia ili kulinda amani ya nchi yetu,” alisema.
Mufti Simba aliweka wazi kuwa katika shughuli hiyo ya kutimiza ibada ya Hijja, Mtanzania mmoja kutoka Mkoa wa Singida alipata matatizo ya afya baada ya kupata tatizo la ubongo lakini alihudumiwa vema na madaktari. Alifafanua kuwa afya ya muumini huyo inaendelea vema na tayari amerejeshwa nchini kuendelea na matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) hadi hali yake itakapotengemaa.
Simba aliongeza kuwa licha ya dosari hiyo kujitokeza Hijja ya mwaka huu imefanikiwa kwa kiasi kikubwa na kuwa sehemu ya kujivunia na kuishukuru Serikali ya Tanzania kwa kufanikisha safari hiyo muhimu. Pia Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum alisema ni vizuri Waislamu wote nchini wakaendelea kudumisha amani na utulivu na kuishi kwa upendo na jamii mbalimbali bila kujali tofauti za dini.
“Waislamu wote waliokuwepo Makkah waliishi kwa upendo na watu wa mataifa mbalimbali duniani hali ambayo inapaswa kuendelezwa nchini ili kudumisha amani na utulivu uliopo kwa maslahi ya taifa,” alisema.
Source: Jambo leo



